MISSION HOUSES


“Our Congregation dedicates itself to the needs of the local and universal Church and devotes itself the Parrochial ministry and other works of the Apostolate which are assumed according to the Provincial, Vicariate and the norms of the Mission.” (NT S11)

Mkiwa Parish

Katika mwaka wake wa Jubilei ya Dhahabu, Jimbo Katoliki la Singida limezindua Parokia mpya ya Mkiwa, na imekuwa Parokia ya thelathini katika Jimbo. Parokia mpya ya Mkiwa imewekwa chini ya ulinzi wa Mt. Ursula Ledochowska ambaye ni mwanzilishi wa Shirika la Masista wa Ursula wa Moyo Mt. wa Yesu Mteswa. Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 27 Januari 2022, kwa Misa Takatifu iliyoongozwa na Mhashamu Baba Askofu Edward Mapunda wa Jimbo Katoliki Singida. Uzinduzi rasmi ulifanyika kwa kusoma hati maalum ya kuanzisha Parokia kadiri ya utaratibu unaoongozwa na Sheria za Kanisa (CCL # 515 ?1-3). Pd. Alessandro Manzi kwa barua ya uteuzi aliyomwandikia Baba Askofu, anakuwa Paroko wa kwanza wa Parokia ya Mkiwa. Pd. Alessandro alisimikwa kwa kiapo maalum na kukiri imani Katoliki mbele ya waamini. Wakili wa Askofu Pd. Francis Limu ndiye aliyesoma hati maalum ya kuisimika Parokia na kutaja mipaka yake na Vigango vinavyoiunda Parokia. Parokia ya Mkiwa inapakana kwa Kaskazini na Parokia ya Ikungi, mashariki inapakana na Parokia ya Manyoni, kwa kusini inapakana na Parokia ya Itigi, magharibi inapakana na Parokia ya Tura. Vigango vinavyoiunda Parokia ya Mkiwa ni Gurungu, Iwerewere, Weruweru na Choda.

abt-img-02

abt-slider-01
abt-slider-01
abt-slider-01

Blessed are you, Virgin Mother! Your Son, Christ Jesus, spotless lamb has prepared for his spouse, the Church, the new bread and wine of the wedding banquet

Umebarikiwa, ee Mama na Bikira; Mwanao Yesu Kristo, Mwanakondoo asiye na doa, alilitayarishia Kanisa, mchumba wake, mkate na divai mpya ya karamu ya arusi

The cup of blessing that we bless is communion with the Blood of Christ. The bread that we break is communion with the body of Christ

(1Cor. 10:16)

Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je, si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, Je, si ushirika wa mwili wa Kristo?

(1Kor. 10:16)

Message From St. Gaspar

“I would rather die or suffer evil than to take such an oath. I cannot, I must not, I will not!” St. Gaspar spent five years in jail for refusing to take the oath"